- Na islam-guide.com
- Maelezo: Jinsi Uislamu unavyofafanua furaha ya kweli na amani moyoni.
Furaha ya kweli na amani inapatikana kwa kutii amri za Muumba na Mtegemezi wa ulimwengu huu. Mungu amesema katika Kurani:
“Kwa kweli, katika kumkumbuka Mungu mioyo hupata raha na utulivu.” (Kurani 13:28)
Kwa upande mwingine, yule ambaye hatakifuata kitabu kitukufu atakuwa na maisha ya shida katika ulimwengu huu. Mungu amesema:
” Atakayeiacha Qur’ani,[1] atakuwa na maisha magumu, na tutamfufua kipofu katika siku ya Kiyama.” (Kurani 20: 124)
Hii inaweza kuwa kielelezo ni kwanini watu wengine hujiua wakati wanafurahia raha ya mali inayoweza kununuliwa na pesa. Kwa mfano, angalia Cat Stevens (sasa Yusuf Islam), zamani alikuwa mwimbaji maarufu wa ‘pop’ ambaye alikuwa akipata zaidi ya dola 150,000 kwa usiku. Baada ya kusilimu, alipata furaha ya kweli na amani, ambayo hakupata katika mafanikio ya mali.[2]